Misri na Djibouti
Jumamosi, 30 Machi 2019
Misri na Djibouti

Historia 

Misri  na  DJibouti zina mahusiano imara ya kihistoria  na ya  kimkakati,wakati ambapo Misri  inazingatiwa kuwa ni  moja ya nchi za kwanza ambazo zilifanya  mahusiano  ya kidiplomasia  pamoja na kufungua ubalozi wake nchini DJibouti baada ya  kupata uhuru katika mwaka 1977, Misri  pia  ilifanya haraka  kwa ajili ya kuyakaribisha makubaliano  ya kisiasa  yaliyosainiwa kati ya serikali  pamoja na umoja wa vyama vya upinzani  nchini DJibouti  kwa ajili ya kumaliza  mgogoro wa kisiasa, kwa upande mwingine  Djibouti imeiunga mkono  Misri katika vikao vya Kimataifa, ambayo hivi karibuni ilikuwa  kupiga kura dhidi ya azimio la baraza la amani na usalama la umoja wa Afrika  kwa kusimamisha ushiriki wa Misri katika shughuli za umoja  wa  Afrika  baada ya  mapinduzi ya Juni 30. Na jambo  ambalo linayaimarisha mahusiano  imara kati ya pande mbili ni eneo la kimkakati  la Jibouti  katika  lango kuu la Bahari ya Shamu karibu na Ghuba ya Adeni na mlango wa Bab El-Mandab kusini mwa lango la Mfereji wa Suez. Na unaozingatiwa kuwa ni  moja ya mihimili mikuu ya usalama wa taifa la Misri pia Djibouti inazingatiwa kuwa ni mlango muhimu wa eneo la pembe ya Afrika na Afrika mashariki kwani  ina  miundombinu pamoja na bandari ya kisasa.

Mahusiano  ya  kisiasa

Ziara  iliyo muhimu ya Rais wa Djibouti, Mhe. Esmail Omar Gila nchini Misri katika mwezi wa Desemba mwaka 2016 imeonesha  mahusiano  imara kati ya nchi mbili, ambapo amefanya  mazungumzo ya kina ya pande mbili pamoja na Rais Abdal Fatah El-Sisi  ambayo yameshughulikia  njia za kuimarisha  pande  mbalimbali za mahusiano ya pande mbili  kutokana na ushiriki wa Mawaziri  wahusika kutoka  pande mbili. Kama walivyojadiliana  baadhi ya maswala ya pamoja  ya Kikanda na Kimataifa, kama walivyozungumzia pia hali ya mambo katika eneo la pembe ya kiafrika na Yemen na hali ya usalama na amani barani Afrika na changamoto ambazo Afrika inakabiliana nazo  kutokana na migogoro kadhaa barani Afrika  pamoja na ongezeko la tishio la ugaidi. Vile vile  Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Djibouti  Mahamoud Ali Yussuf alitembelea  Misri  tarehe 8 ya mwezi wa Novemba mwaka 2017, na katika ziara yake hiyo  amekutana na Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Misri Sameh Shukri, ambapo  walifanya mazungumzo kuhusu mahusiano ya pande mbili kati ya nchi mbili na maswala ya eneo la pembe ya Afrika na kuanzisha utaratibu  wa mashauriano  ya kisiasa  ya mara kwa mara kati ya nchi mbili  kwa upande wa Mawaziri wa Mambo ya Kigeni.

Mahusiano  ya  kiuchumi

Licha ya kuwepo kwa mahusiano imara kati ya Misri na Djibouti isipokuwa  kiwango cha kubadilishana  biashara  kati ya nchi mbili hakivuki dola za kimarekani milioni 30 kila mwaka hazioneshi nguvu za mahusiano imara kati ya nchi mbili, licha ya ziara ya Rais wa Djibouti nchini Misri katika Desemba mwaka 2016 iliyoshuhudia utilianaji saini  mikataba kadhaa na hati za mashirikiano muhimu katika nyanja mbalimbali  ambazo zilijumuisha :

 Hati ya makubaliano ya kusafirisha na kuagiza na kuvuka mifugo na nyama , na hati ya makubaliano ya uwanja wa elimu ya kiufundi, na hati ya makubaliano ya mashirikiano ya uwanja wa ushiriki wa maonesho na masoko ya kimataifa ,na hati ya makubaliano ya uwanja wa mashirikiano ya kibiashara na mikataba ya mashirikiano ya kiuchumi na ya kiufundi kati ya nchi mbili, na hati ya makubaliano ya uwanja wa afya na madawa pamoja na hati ya makubaliano kati ya mamlaka ya Mfereji wa Suez na Mamlaka ya Bandari za Djibouti. Pia Nchi mbili zina makubaliano ya mashirikiano  ya pamoja, na hati za makubaliano katika Nyanja mbalimbali. Na idadi yake inakadiriwa kwa mikataba na hati za makubaliano 33, Pia tume ya pamoja ya mashirikiano ya kiuchumi na ya kiufundi ya nchi mbili  imefanya vikao kadhaa, kupatikana wawekezaji wa kimisri nchini Djibouti kutoka Makampuni mawili ya  Umoja wa Wahandisi na ambao kwa  sasa wanafanya miradi mbalimbali katika uwanja wa ujenzi  na Jumuiya ya Shoura ambayo imeweza kuanzisha benki ya Misri nchini Djibouti.

 

Mahusiano ya kiutamaduni

 AL- Azhar Sharif na Vyuo Vikuu vya Misri vinatoa mchango muhimu katika kuimarisha mahusiano ya kiutamaduni kati ya nchi mbili, Na hayo ni kutokana na  mapokezi ya Misri  kwa nafasi za masomo za Djibouti, pia Misri inatoa fursa kadhaa za kutoa mafunzo kwa ajili ya wenye vipaji wa Djibouti katika nyanja mbalimbali, na hayo yanatimia kutokana na programu ya kutoa mafunzo inayotolewa na Shirika la Misri kwa ushirikiano wa maendeleo. Idadi ya wajumbe  wa  AL- Azhar Sharif  kwa sasa inakadiriwa wajumbe 12 ukiongezea na nafasi za masomo  zinazotolewa na AL- Azhar kwa ajili ya wanafunzi wa Djibouti, na ambayo idadi yake inakadiriwa nafasi15 kila mwaka   na idadi ya  wataalamu wa mfuko wa Misri wa ushirikiano wa kiufundi pamoja na Afrika nchini Djibouti inakadiriwa wataalamu 12 katika  nyanja kadhaa. Na wizara ya elimu ya juu imekubali ombi la Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Djibouti kwakuongeza la idadi ya nafasi za Vyuo Vikuu na masomo ya Juu maalumu kwa Djibouti  hadi kufikia nafasi15 ukiongezea na nafasi10 za masomo ya juu ili kufaika katika mwaka wa masomo, 2016 /2017.

Mahusiano ya Kijeshi

Hakika  Misri inatoa  mafunzo ya kiufundi na masomo ya kijeshi  ndani  ya vyuo vyake  vya kijeshi kwa makanda wa kijeshi  wa Djibouti katika nyanja mbalimbali. Ukiongezea na misaada ya Misri kwa DJibouti katika uwanja wa kupiga vita ugaidi na msimamo mkali kutokana na  kuziboresha mbinu zinazotumika kwa ajili ya kuimarisha  mahusiano ya mashirikiano ya kijeshi na ya usalama pamoja na kulinda eneo la bahari ya Shamu kutokana na vitisho vya ugaidi pamoja na uharamia wa kimataifa.